Find us on facebook

Pages

Follow Me.

Saturday, June 1, 2013

ZANA ZA HIZBOLLAH ZAPATIKANA NIGERIA.

Karakana ya silaha inayoaminika kumilikiwa na kundi la Hezbollah, nchini Lebanon imapatikana Kaskazini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi na shirika la ujasusi la Nigeria
raia watatu wa Lebanon wamekamatwa. Msemaji wa jeshi, Brigedia Gen Ilyasu Isa Abba, pia amethibitisha hilo.

Maafisa wa usalama walisema kuwa silaha hizo zilinuiwa kutumiwa dhidi ya maslahi ya Israel na nchi za Magharibi.Silaha hizo ikiwemo, risasi, zana za kukinga magari ya kivita dhidi ya mashambulizi na RPG, zilipatikana ktika karakana mjini Kano.
Hii ni kazi ya Hezbollah," katibu mkuu wa usalama mjini Kano Bassey Ettang alisema.Na unaweza hata kuwa na uhakika kuwa ikiwa hili linafanyika, inawezekana wanasaidia makundi ya kigaidi wanaoendesha harakati zao nchini humu,'' alidokeza bwana Bassey.
Brig Gen Ilyasu Isa Abba alisema kuwa zana 11 za magari ya kivita, guruneti na makombora 21 bunduki 17 aina ya Ak-47 na maguruneti 76 ni baadhi ya silaha zilizopatikana.
Mmiliki wa karakana hiyo, ambako silaha zilipatikana, zikiwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao, hakuwa nchini humo.
Kuna jamii kubwa ya walebanese wanaofanya kazi mjini Kano, mji wa kibiashara wa Nigeria Kaskazini.
Mji wa Kano eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zimekubwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika miaka mitatu iliyopita, tangu wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram walipoanzisha harakati zao.
Bwana Ettang aliongeza kuwa "unaweza pia kuwa na uhakika kundi kama hili likiwa lipo, inaweza hata kuwasaidia wapiganaji wengine walioko nchini humo.''
Hezbollah ni kundi la Kishia pamoja na kuwa vuguvugu la kisiasa lenye makao yake nchini Lebanon. Linatambulika na Marekani kama kundi la kigaidi.
Boko Haram, ambalo jina lake lina maanisha tamaduni za kimagharibi zinapingwa, linasema, nia yake ni kuipindua serikali sasa na kubuni serikali ya kiisilamu.
Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kundi la Boko Haram huenda linasaidiwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda katika nchi zengine

No comments:

Post a Comment